Kuhusu Sisi

Alama Group Ministry ni matokeo ya ndoto ya kuwasaidia watoto yatima na familia zinazoishi katika mazingira magumu. Baada ya kumshirikisha Mungu  kuhusu maono hayo, akaaonesha njia na namna ya kuanza kuiendea kwa kidogo alichowezesha kuwa nacho an kuahidi kwamba yeye ndiye akuzae.

Furaha yangu na wajibu wangu ni kumsikiliza Muumba na kumcha yeye siku zote. Katika maneno hayo nina kila sababu ya mimi kuishi kwa utukufu wa jina lake na uweza wake ukawafikie mataifa na kuwaonehsa upendo ambao Bwana alituachia na kutusihi kwamba tupendane siku zote. Tangu misingya uumbaji hapo mwanzo Mungu aliweka kila jambo na mali zote ambazo mwanadamu anahitaji. kwa hiyo kwa msaada wake tutazalisha katika mimea na wanyama na kuonesha uwezo wa kumiliki na kutawala kwa mfano wa Mungu.

Ungana nasi katika mipango yetu kwa kupiga simu namba +255 759 61 27 61